NYASA TOURISM FESTIVAL

NYASA TOURISM FESTIVAL

Thursday 29 September 2016

SAMAKI WA MAPAMBO NYASA NI RASILIMALI ADIMU

Samaki wa mapambo ambao wanapatikana kwa wingi katika eneo la Liuli ziwa Nyasa wanaweza kubadilisha maisha ya wakazi wa mwambao mwa ziwa Nyasa.Inadaiwa samaki mmoja wa mapambo nje ya nchi anauzwa hadi dola za Marekani 500.Leonard Nkomola ni mvuvi wa kuzamia samaki hao tangu mwaka 1993 katika eneo la Liuli,anasema kampuni zimekuwa zinauza samaki hao katika nchi za Ujerumani,Afrika ya Kusini,Ufaransa na Norway.Anasema kwa mwaka wana uwezo wa kukamata samaki wa mapambo hadi 10,000.Utafiti umebaini katika eneo la Liuli kuna aina 125 za samaki wa mapambo.Maeneo mengine katika ziwa Nyasa ambako samaki wa mapambo wanapatikana ni Kyela Mkoa wa Mbeya na Ludewa Mkoa wa Njombe.

No comments:

Post a Comment